![]() |
| Pakistan yaokoa familia iliyotekwa na Taliban miaka 5 iliyopita |
Jeshi la Pakistan limeiokoa familia moja ya watu watano raia wa Marekani ambao walikuwa wakishikwa mateka na wanamgambo wa Taliban wa Afghanistan.
Waliokolewa wakati wa oparesheni katika wilaya moja yenye makabila ya Kurram karibu na mpaka na Afghanistan.
Jeshi la Afghanistan halikuitaja familia hiyo, lakini raia wa Canada Joshua Boyle na mkewe raia wa Marekani Caitlan Coleman, walitekwa walipokuwa wakitembea nchini Afghanistan mwaka 2012.
Wanaaminika kupata watoto wakiwa mateka.
![]() |
| Pakistan yaokoa familia iliyotekwa na Taliban miaka 5 iliyopita |
Video ya mwisho ya wawili hao ilitolewa Disemba mwaka uliopita wakati walionekana wakiomba nchi zao kuwaokoa.
Walionekana wakiwashika watoto wao wadogo wa kiume waliozaliwa wakiwa wameshikwa mateka.


Comments
Post a Comment