Zaidi ya 300 wajeruhiwa wakati wa kura ya uhuru Catalonia


Maafisa huko Catalalonia wanasema kuwa watu 337 wamejeruhiwa kwenye ghasia wakati polisi wanajaribu kuzuia kura ya maoni ya uhuru wa Catalonia

Zaidi ya 300 wajeruhiwa wakati wa kura ya uhuru Catalonia
Serikali ya Uhispania imeahidi kuzuia kura hiyo ambayo imetangazwa kuwa isiyo halali na mahakama ya katiba ya nchi hiyo.
Polisi watibua jaribio la pili la shambulio Uhispania
Maafisa wa polisi wanawazuia watu kupiga kura huku wakichukua makaratasi ya kupigia kura na masanduku kutoka kwa vituo vya kupigia kura.

Makatasi ya kipigia kura yana swali moja tu: "Unataka Catalonia kuwa taifa huru na jamhuri?" Kuna masanduku mawili ya ndio na hapana.



Katika mji wa Girona polisi wa kuzima ghasia waliingi katika vituo vya kupigia kura kwa nguvu ambapo kiongozi wa eneo hilo alitarajiwa kupigia kura yake.
Washambuliaji wa Barcelona walipanga kutumia mitungi 120 kwenye mashambulizi
Picha za televisheni ziliwaonyesha wakivunja vioo vya kuingia kituo hicho na kuwaondoa kwa nguvu wale waliojaribu kupiga kura.

Hata hivyo shirika la habari la Reuters lilisema kuwa Bw Puigdemont alifanikiwa kupiga kura yake.
Wakati huo huo kwenye mji mkuu wa eneo hilo, Barcelona polisi walifyatua risasi za mipira kwa wale wanaounga mkono hatua ya kujitenga.

Comments